106. Mungu awe nanyi daima

 1. Mungu awe nanyi daima,

Hata twonane ya pili,
Awachunge kwa fadhili,
Mungu awe nanyi daima.

 Hata twonane huko juu,
 Hata twonane kwake kwema;
 Hata twonane huko juu,
 Mungu awe nanyi daima.
          
2. Mungu awe nanyi daima;
Ziwafunike mbawaze,
Awalishe, awakuze;
Mungu awe nanyi daima.

3. Mungu awe nanyi daima;
Kila wakati wa shani
Awalinde hifadhini;
Mungu awe nanyi daima.

4. Mungu awe nanyi daima;
Awabarikie sana,
Awapasulie kina;
Mungu awe nanyi daima

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu