107. Ewe, Baba wa Mbinguni

 1. Ewe, Baba wa Mbinguni,

Usikie twombalo
Hapa chini duniani,
Na uwe radhi nalo

 Ee Mungu, bariki
 Ndugu hawa wawili!
 Ee Mungu, bariki
 Ndugu hawa wawili!
          
2. Watu hawa mbele zako,
Na mbele ya kanisa;
Watimize Neno lako
Wanakutana sasa.

3. Kama Yesu na Kanisa,
Ni mmoja, na hivyo,
Watu hawawape sasa
Wawe mmoja vivyo

4. Walinde, Bwana, daima,
Wabariki nyumbani
Uwape nyingi salama
Humu ulimwenguni.

5. Wabariki, ewe Bwana,
Watu hawa wawili,
Wape upaji wa wana,
Wafurahishwe kweli.

6. Siku za duniani
Zitakapopungua,
Wape kurithi Mbinguni
Mema ya kwendelea.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu