117. Tufani inapovuma

 1. Tufani inapovuma

Sana moyoni mwangu,
Huona pa kujificha
Mkononi mwa Mungu.

 Hunificha, hunificha
 Adui hatanipata,
 Hunificha, hunificha,
 Mkononi mwake.
          
2. Pengine kuna taabu
Yanisongeza kwake;
Naijua si hasira,
Ni ya mapenzi yake.

3. Adui wakiniudhi
Nami nikisumbuka,
Mungu atavigeuza
Vyote viwe baraka.

4. Niishipo duniani
Ni tufani daima,
Anilindapo rohoni
Nitakaa salama.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu