132. Sauti sikilizeni

 1. Sauti sikilizeni

Za waimbao juu,
“Aleluya, Aleluya,
Aleluya, mkuu!”
Wako makundi-makundi
Kama nyota wang’ara,
Kwa makuti ya mitende,
Na meupe wamevaa.

2. Wazazi na manabii
Wafanyaji wa njia;
Mashahidi, waandishi,
Nao wafalme pia!
Mabikira kina-mama,
Wajane wa kusali,
Waimba wakikutana
“Msifunu Imanweli”.

3. Watu toka huzunini
Wameosha na nguo,
Ni kwa damu yake Yesu;
Maonjo, mbali nao!
Walitekwa, walikatwa
Hata kwa misumeno,
Kwao kifo na shetani
Walishindiwa mno.

4. Mungu mumo mwake Mungu,
Nuru mumu mwa nuru,
Kwa kufungamana mwako
Tutaishi mahuru;
Tujalize, Imanweli,
Kujaa kwako wewe
Mungu Baba, Mungu Mwana,
Mungu Roho, tunawe

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu