134. Juu yake langu shaka

 1. Juu yake langu shaka,

Yesu namuwekea,
Nami sitafedheheka
Nikimtegemea.

 Natumai, natumai,
 Nnatumai kwake tu;
 Natumai, natumai,
 Natumai kwake tu.
          
2. Juu yake, dhambi zangu;
Aniosha kwa damu;
Nionekane kwa Mungu,
Nisiye na laumu.

3. Juu yake yangu hofu;
Kwake nimetulia;
Sipotei kwa upofu
Njia aning’azia.

4. Juu yake raha yangu;
Humuangalia tu;
Mwenye kila ulimwengu,
Aniruzuku na huu.

5. Juu yake, moyo wangu;
Hali yangu na mali;
Mimi wake, Yeye wangu,
Twapasana kamili.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu