139. Nuru ya Rohoni
1. Nuru ya rohoni
ni Bwana Yesu.
Nakuomba sana
niangazishe;
ukanitazame
kwa huruma tu,
/: ukanitulize
mimi maskini. :/
2. Futa dhambi zangu
kwa damu yako.
Hasira ya Mungu
iniondoke.
Machubuko yako,
hata mateso,
/: niyawaze vema
rohoni mwangu. :/
3. Nakutumaini
peke yako tu,
niwe mtumwa wako
pote nilipo
utanikubali
sina mashaka!
/: Nitakushukuru
pasipo mwisho. :/
Comments
Post a Comment