139. Nuru ya Rohoni

 1. Nuru ya rohoni

ni Bwana Yesu.
Nakuomba sana
niangazishe;
ukanitazame
kwa huruma tu,

 /: ukanitulize
 mimi maskini. :/

2. Futa dhambi zangu
kwa damu yako.
Hasira ya Mungu
iniondoke.
Machubuko yako,
hata mateso,

 /: niyawaze vema
 rohoni mwangu. :/

3. Nakutumaini
peke yako tu,
niwe mtumwa wako
pote nilipo
utanikubali
sina mashaka!

/: Nitakushukuru
 pasipo mwisho. :/

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu