145. Ndoa Yetu Nzima
1. Ndoa yetu nzima
simika, Yesu!
Usiku na mchana
uwepo kwetu.
Leo tuna raha,
Wewe watupa.
/:Ndoa yetu Bwana
ndiwe Baraka!/:
2. Atoka kijana,
ataka mchumba
siku zinapita
za kupimana.
Leo twapatana
pamoja kukaa
/:Ndoa yetu…:/
3. Vyote hapa chini
vinakaa muda,
vyote vinaoza,
tena vyachakaa.
Pendo la duniani
nalo huchakaa
/:Ndoa yetu…/:
4. Kakaa kwetu Bwana,
kutukagua,
pendo letu sisi
lisichakae:
Hivi na tukae
na baraka tu.
/: Ndoa yetu…:/
5. Kana arusuni
ulialikwa,
walivyoishiwa
ukaongeza,
nasi shida zetu
utazishinda.
/:Ndoa yetu..:/
Comments
Post a Comment