6. Baba Mwana Roho


1. Baba, Mwana, Roho,
Mungu mwenye enzi,
Kila tukiamka tunakuabudu
Baba, Mwana,
Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.

2. Baba, Mwana, Roho, wakuaminio
Wanakutolea shukrani zao
Wanakusujudia malaika nao:
Wewe u mwanzo, nawe u mwisho.

3. Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,
Utukufu wako hatuoni kosa;
U Mtakatifu, nawe u mapenzi,
U peke yako, mwenzio huna.

4. Baba, Mwana, Roho,
Mungu mwenye enzi,
Ulivyoviumba vyote vyakusifu:
Baba, Mwana, Roho,
Mungu wa mapenzi
Ewe Utatu, tunakusifu.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu