65. Safari

 1. Katika safari yetu

Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini.

 Ng’oani!  Tujifungeni,
 Twende zetu juu!
 Kristo ndiye kiongozi;
 Tusihofu tu.
          
2. Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.

3. Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.

4. Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.

5. Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu