67. Bwana uliyewaita

 1. Bwana uliyewaita

Watakatifu wako,
Wawe mitume, wachunga,
Walishe kundi lako;
wanyonge na wenye hofu
Wakawa mashujaa,
Na wapole wa kunena
Wasiwe kunyamaa.

2. Hata leo wawataka
Watakatifu wako,
Nawe wauliza tena
Ni nani aliyeko
Atakaye nimtume
Afundishe vijana?
“Ni tayari, Bwana wangu,
Nitume mimi Bwana.”

3. Nitume na mimi, Bwana
Kama ulivyotumwa,
Habari ya msamaha
Na dhambi kutubiwa,
Na waliopotea,
Wokovu u wake Bwana,
Aliyewafilia.

4. Astahiliye hapana
Kutamka habari,
Lakini wewe waweza
Kutufanya tayari.
Neno lako tulijue,
Tupe na roho yako,
Hayatakuwa ya bure,
Haya maneno yako

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu