70. Yesu atuchunga

 1. Yesu atuchunga,

Mchunga wetu,
Naye atufuta
Machozi yetu;
Mkononi mwake
Hatuna hofu,
Daima twapata
Kwake wokovu.

2. Yesu atuchunga
Tumemjua,
Na sauti yake
Twaitambua;
Naye akituonya
Ni kwa upole,
Tu kondoo zake
Hata milele.

3. Yesu atuchunga;
Aliwafia
Kondoo wakubwa
Na wana pia;
Kwamba awajua,
Kondoo zake,
Hutiwa alama
Ya damu yake.

4. Yesu atuchunga;
Mikono yake
Imewaambata
Kondoo zake;
Hapati wadhuru
Adui yule,
Yesu awalinda.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu