75. Waimba, sikizeni

 1. Waimba, sikizeni,

alaika Mbinguni;
Wimbo wa tamu sana
Wa pendo zake Bwana,
“Duniani salama,
Kwa wakosa rehema.”
Sisi sote na twimbe
Nao wale wajumbe;
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.

2. Ndiye Bwana wa Mbingu,
Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili,
Mwana wa mwanamwali;
Ametoka enzini
Kuja ulimwenguni
Mwokozi atufie,
Ili tusipotee.
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.

3. Mtukufu wa amani
Ametoka Mbinguni,
Jua la haki, ndiye
Atumulikiaye;
Amejivua enzi,
Alivyo na mapenzi,
Ataka kutuponya,
Kutuzalisha upya,
Waimba sikizeni,
Malaika Mbinguni.

4. Njoo upesi, Bwana,
Twakutamani sana;
Kaa nasi, mwokozi
Vita hatuviwezi;
Vunja kichwa cha nyoka,
Sura zako andika,
Tufanane na wewe,
Kwetu sifa upewe,
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu