78. Sioshwi dhambi zangu

 1. Sioshwi dhambi zangu,

Bila damu yake Yesu.
Hapendezewi Mungu,
Bila damu yake Yesu.

 Hakuna kabisa
 Dawa ya makosa
 Ya kututakasa,
 Ila damu yake Yesu.
          
2. La kunisafi sina
Ila damu yake Yesu.
Wala udhuru tena,
Ila damu yake Yesu.

3. Sipati pataniswa,
Bila damu yake Yesu.
Hukumu yanitisha,
Bila damu yake Yesu.

4. Sipati tumaini,
Bila damu yake Yesu.
Wema wala amani,
Bila damu yake Yesu.

5. Yashinda ulimwengu,
Hiyo damu yake Yesu.
Na kutufikisha juu,
Hiyo damu yake Yesu.

6. Twaimba: Utukufu
na damu yake Yesu.
Milele twaisifu,
Hiyo damu yake Yesu.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu