90. Aliteswa Aliteswa


1. Aliteswa, aliteswa,
Msalabani Yesu aliteswa,
Dhambi zangu ameziondoa,
Mahali pangu aliumizwa.

2. Alikufa, alikufa,
Msalabani Yesu alikufa,
Kwa kifo chake nakombolewa,
Kwa kuwa Yesu alinifia.

3. ’Kafufuka, ‘kafufuka,
Kaburini Yesu alitoka,
Nami nimewekwa huru pia,
kwa kuwa Yesu alifufuka.

4. Yuko hai, yuko hai,
Mbinguni anaishi Mwombezi,
Daima huniombea mimi,
Kwa kuwa Yesu adumu hai.

5. Atarudi, atarudi,
Siku moja Yesu atarudi,
Na tutamwonapo tutafurahi,
Kwa kupelekwa kwake Mbinguni.

6. Sifa kwake, sifa kwake,
Mbinguni na huimbwa milele,
Kwa furaha, masifu, na shangwe,
Tutamwimbia Yesu milele.

Comments

Popular posts from this blog

52. Yote namtolea Yesu

85. Ni Mtu wa Simanzi

48. Naweka dhambi zangu